Wednesday 4 November 2015

MIMBA KUTUNGA NJE YA KIZAZI (ECTOPIC PREGNANCY)


MIMBA KUTUNGA NJE YA KIZAZI (ECTOPIC PREGNANCY)


Kiasi cha asilimia 2 ya mimba zote hutungwa nje ya mji wa uzazi. Hali hii hujuilikana kama ectopic pregnancy kwa kiingereza au extrauterine pregnancy kwa kitaalamu. Mara nyingi mimba zinazotunga nje ya kizazi huwa haziwezi kukua mpaka mwisho wa ujauzito, huweza kuleta hatari kwa afya ya mama hasa pale inapopasuka na kuvujisha damu tumboni mwa mama.

Namna Mimba Za Nje ya Kizazi Zinavyotokea

Kwa kawaida mbegu ya kiume na yai la kike hukutana katika mirija ya uzazi (Fallopian tubes) na mimba hutungwa. Kiinitete husafri polepole kwenda kwenye mji wa uzazi ambako hujipandikiza kwenye ukuta wa uzazi na mimba huanza kukua. Katika ugonjwa huu wa mimba kuwa nje ya kizazi (ectopic pregnancy) mbegu ya kiume na yai huungana kutengeneza kiinitete. Badala ya kupandikizwa kwenye tumbo la uzazi, kiinitete huenda kujipandikiza sehemu nyingine tofauti na mji wa uzazi. Kinaweza kujipandikiza kwenye mirija ya uzazi, ovari, kwenye shingo ya uzazi na ndani ya tumbo (abdominal cavity). Mimba nyingi za nje ya kizazi hujipandikiza kwenye mirija ya uzazi ambapo huwa na hatari ya kupasuka kadri mimba inavyokua.
mimba nje ya kizazi (ectopic prgnancy)
mimba nje ya kizazi (ectopic prgnancy)
Mara chache sana mimba zinazotunga nje ya kizazi huweza kukua mpaka mwisho, nyingi huishia kupasuka na kuondolewa kwa upasuaji.

Sababu Hatarishi za Mimba Kutunga Nje ya Kizazi

Zifuatazo ni baadhi ya sababu zinazochangia kutokea kwa mimba za nje ya kizazi.
Ingawa wakati mwingine zinazoweza kutokea bila sababu maalum kujulikana.

Dalili

Kufuatia wiki kadhaa baada ya kukosa siku zako za hedhi, unaweza kuanza kupata maumivu ya tumbo chini ya kitovu au kiuno, ambayo yanaweza kuwa upande mmoja. Maumivu yanaweza kuja na kuacha, kuwa makali sana kiasi cha kushindwa kuvumilia.
Hali hii inaambatana na kutokwa damu ukeni, mara nyingi ikitoka kidogo kidogo. Inaweza kuwa nyepesi au nzito nyeusi.
Wakati mwingine unaweza usipate dalili zozote, tatizo likagunduliwa wakati wa kipimo cha ultrasound. Kuna baadhi ya watu wanaweza wasipate dalili zozote na mimba kukua nje ya kizazi mpaka wakati wa kujifungua kukaribia.

Vipimo

Tatizo hili hugunduliwa kwa kipimo cha ujauzito (kwa mkojo au damu) kuthibisha kama mtu ana mimba na kisha ultrasound ya tumbo ili kuona mimba ilipo.
Kipimo cha mimba. Kipimo cha mimba cha mkojo (urinary pregnancy test) au cha mimba cha damu (serum HCG) hufanyika kuthibitisha uwepo wa mimba.
Ultrasound ya tumbo. Hii hufanyika kuonesha mimba ilipo. Wakati mwingine kwa wiki za mwanzoni (chini ya wiki 5) mimba iliyo nje ya kizazi inaweza kuwa ngumu kuiona kwenye ultrasound. Kama ipo nje ya kizazi au imepasuka itaonekana kwa kipimo hiki.

Matibabu

Matibabu ya mimba nje ya kizazi yanaweza kuwa ya dawa peke yake au kwa njia ya upasuaji. Matibabu ya dawa huanzishwa pale ambapo mimba ni ndogo na viwango vya hcg kwenye dami si vikubwa sana. Unaweza ukapewa dawa moja au mchanganyiko na ukawekwa kwenye ufuatiliaji wa karibu mpaka utakapopona.
Matibabu ya upasuaji hufanywa pale mimba inapopasuka, kuwa kubwa au mara chache imekomaa karibu na kujifungua. Upasuaji huusisha kuuondoa mimba iliyo nje ya uzazi, kama mirija imehusika basi kukata sehemu iliyoharibika na kuunganisha tena. Wakati mwingine mirija huondolewa moja kwa moja. Kwa mtoto ambaye ameshakomaa, tumbo hupasuliwa na mtoto kuondolewa.

Kupata Ujauzito Tena
Kwa wanawake wanaotarajia kupata tena ujauzito baada ya matibabu ya mimba kutunga nje ya uzazi, huweza kupata ujauzito wa kawaida. Ila kuna mambo matatu;
  • kupata mimba ya kawaida,
  • mimba kutunga tena nje ya kizazi au
  • kupata ugumba.
Kama uliwahi kupata mimba nje ya uzazi kabla ya hii, maambukizi kwenye mirija ya uzazi, upasuaji kwenye mirija ya uzazi au historia ya ugumba huongeza uwezekano wa tatizo kujirudia au kuwa mgumba.
Unaweza kupata ujauzito wa kawaida baada ya mimba kutunga nje ya kizazi. Zaidi ya asilimia 80 ya wanawake huenda kupata ujauzito wa kawaida baada ya kupona.


No comments:

Post a Comment