Wednesday 4 November 2015

Dalili na ishara za Ujauzito


Dalili na ishara za Ujauzito:

1. Kutokwa damu kidogo ukeni wakati kiumbe kikipandikizwa kwenye mfuko wa uzazi, ingawa siyo wanawake wote hupatwa na dalili hii 

2. Kukosa hedhi, hii ni moja ya dalili kubwa za ujauzito 
3. Maumivu ya matiti na kuvimba matiti (huweza kutokea kati ya wiki ya 1 hadi ya 2) 
4. Uchovu, wanawake wengi hujihisi uchovu na hali ya kutopenda kufanya lolote. 
5. Kupoteza ladha au kuhisi ladha ya chuma mdomoni 
6. Kuongezeka kwa hisia ya harufu, kipindi cha ujauzito wanawake wengi huongezeka hisia ya harufu 
7. Kichefuchefu na kutapika 
8. Maumivu ya kichwa 
9. Kizunguzungu 
10. Kukojoa mara kwa mara (hasa kati ya wiki 6-8) 
11. Kubadilika rangi kwa ngozi inayozunguka chuchu kuwa nyeusi 
12. Kutamani baadhi ya vyakula na kuchukia vingine 
13. Kupanuka kwa mfuko wa uzazi 
14. Tumbo kujaa au kuvimbiwa 
15. Kununa na kukasirika haraka 
16. Kiungulila au kupata choo kigumu 
17. Kolostramu kuanza kutoka kwenye matiti 
18. Kuongezeka uzito 
19. Kuweza kupapasa mtoto (palpation of the baby) 
20. Kulainika na kuvimba kwa shingo ya uzazi (Hegars sign) - kuanzia wiki ya 6 
21. Shingo ya uzazi kubadilika rangi kuwa ya samawati kutokana na msongamano wa damu katika mishipa ya vena. Ishara hii huitwa pia Chadwick's sign

Dalili nyingine ni pamoja na 


1. Mstari wima mweusi hutokea tumboni kuanzia chini ya kitovu (linea nigra) 
2. Mama kuhisi mtoto akicheza (kuanzia wiki ya 20) 
3. Maumivu ya mgongo hasa mimba ikishakuwa kubwa. 
4. Kipimo cha mimba kuwa chanya (positive). 
5. Kusikia mapigo ya moyo ya mtoto 
6. Mtoto kuonekana kwenye kipimo cha ultrasound 


No comments:

Post a Comment