Tuesday 29 December 2015

SMS NZURI KWA UMPENDAYE

Furaha ni kawaida yangu, kununa si busara kwangu, kuishi nawewe vizuri ni sehemu ya Maisha yangu, kukusalimia ni hulka ya Moyo wangu, Uhali gani mpenzi?


Salamu yako ni nusu ya uhai wangu, kuikosa nisawa na kuidhulumu nafsi yangu, kuipata nisawa na ua ridi machoni mwangu, nakila ninapoipata huwa najisikia faraja moyoni mwangu, Nakupenda sana Muhibu wangu.


Usiku wa leo uwe ni wenye faraja kwako, utawaliwe na usingizi wa mahaba kwenye kope zako, naomba ujenge taswira yangu katika mawazo yako, Usisahau kuniota sweet wangu. USIKU MWEMA 


Fungua macho yako uone kopa za mahaba ninazokumwagia, fungua mikono yako na upokee mapenzi yangu, fungua simu yako uone ni jinsi gani ninavyokukumbuka japo kwa kukutumia sms mpenzi wangu, Nakutakia usiku mwema


Utamu wako ni zaidi ya asali, ni wa asili usiohitaji kuongezewa ladha ya sukari, nitaumiss endapo kama ukiwa mbali "NIACHE NIKUPENDE SWEET"


Moyo wangu umehifadhi hisia zako, nakuahidi kamwe sintopunguza upendo kwako, tunza sms hii ya ahadi kwenye simu yako, iwe kumbukumbu kila uisomapo! "NAKUPENDA MALAIKA WANGU"

Si vibaya mimi kukusifia kwani wewe ni wangu, nivingi umejaaliwa, vinavyouvutia moyo wangu, ama hakika uzuri wako umedhibiti matamanio yangu "SINTOMPENDA MWINGINE ZAIDI YAKO" 


Thamani ya Mapenzi yako nikubwa kwangu, haifanani nachochote kwenye huu ulimwengu, sina budi kumshukuru mungu, kwa kunijaalia mpenzi mwema unaejali hisia zangu, USICHOKE KUNIPENDA MPENZI


Mpenzi kila tunapokuwa chumbani huwa napenda kuwa mbunifu, huwa najitahidi kuepuka udhaifu, ili mapenzi yangu yasikukifu, ENDELEA KUFURAHIA MAPENZI YANGU. Mchana mwema


Wewe ni wapekee ninaekupenda, sifikirii kukusaliti na wala sina wazo la kukutenda, nakuomba tuendelee kupendana siku zote habbity wangu


Mapenzi ni matamu napia yana raha, wewe hauni ishi hamu, siku zote wanipa raha, wewe kwangu ni mtu muhimu, unaeng'aa moyoni mwangu kama nyota ya jaha. "NAKUOMBA USINIACHE MPENZI WANGU"


Pokea sms yangu iliyojaa utamu, nimeipamba kwa maneno laini yenye ladha adimu, utamu wake ni kama apple haufanani na ndimu, nimeituma kwako sms hii ikuletee salamu "UHALI GANI MPENZI?"


Dhamira kuu ya Moyo wangu ni Mapenzi, kukupenda kwa dhati bila kipingamizi, kuishi nawewe kihalali kwa kudra za wazazi, Nipende nikupende Tudumishe Mapenzi. "NAKUTAKIA MCHANA MWEMA MPENZI WANGU"

Katika hadithi zile za kale,
Watu walipendana nyakati zile,
Kwa mapenzi matamu yenye ukweli,
Mapenzi yao hayakujali mali,
Mapenzi yao yalipendeza sana,
Mapenzi yao ya kuaminiana,
Mapenzi yale mie nayatamani,
Ninayahitaji kutoka moyoni,
Ninajuwa mapenzi hayachagui,
Yanapojenga moyo wenye uhai,
Kuna mioyo inajuwa kupenda,
Mapenzi yake hayawezi kupinda,
Mapenzi yawezayo kukuzuzuwa,
Mapenzi moyoni yaliyotulia,
Mapenzi halisi ninayoyaimba,
Ambayo kutoka kwako nayaomba.

Njoo sogea nipe pendo la dhati,
Mapenzi ya uwongo siyafuati,
Njoo kwangu mpenzi we usisite,
Nami nitakupa moyo wangu wote,
Nikisema hivi utanisikia,
Nikitaka hiki utanipatia,
Kumbuka siku ya kwanza nilisema,
Nakupenda wewe tu hadi kiama,
Nikaandika tungo kwa ajili yako,
Nikaonesha mapenzi yangu kwako,
Ndivyo hivyo kamwe sitobadilika,
Nitakupenda pasipo kukuchoka,
Mapenzi yangu kwako usiyakwepe,
Naomba mapenzi halisi unipe,
Kwangu wewe usiwe na wasiwasi,
Nami nitakupa mapenzi halisi.



Siogopi kukupenda, hata watu wakisema,
Kukukosa ninakonda, mwilini ninayo homa,
Moyo mbio wanienda, nisikwone siku nzima,
Siogopi kukupenda, hata watu wakisema.

Moyo wangu una wewe, tele tele umejaa,
Ningepatwa na kiwewe, kama ungenikataa,
Mapenzi yote nipewe, nipende kila wasaa,
Siogopi kukupenda, hata watu wakisema.

Maneno nishasikia, yapo tokea kitambo,
Kwa wivu wanaumia, kukukosa ee mrembo,
Kwangu umesharidhia, huhitaji tena nyimbo,
Siogopi kukupenda, hata watu wakisema.

Waseme yote mchana, walale hapo usiku,
Mioyo yawanyongona, imejaa dukuduku,
Sisi tunavyopendana, wamebaki zumbukuku,
Siogopi kukupenda, hata watu wakisema.

Raha kwako naipata, hakika nimeridhika,
Kwako hakuna matata, moyo wangu umefika,
Usiku ninakuota, kwako naliwazika,
Siogopi kukupenda, hata watu wakisema.

Upendo uso kipimo, wewe nimekupatia,
Moyo unalo tuwamo, raha naipata pia,
Kwenye moyo wangu umo, raha yangu ya dunia,
Siogopi kukupenda, hata watu wakisema.

Wenye kusema waseme, waseme hadi wachoke,
Roho zao ziwaume, ziwaume wakereke,
Mioyoni ziwachome, wachomeke wakauke,
Siogopi kukupenda, hata watu wakisema.

Wenye wivu uwashike, uwashike uwagande,
Zaidi wahuzunike, wahuzunike wakonde,
Chakula kisiwashuke, wacha mie nikupende,
Siogopi kukupenda, hata watu wakisema.

Ni raha mwangu moyoni, wewe kuwa ndiwe wangu,
Nimezama furahani, rahani chini ya mbingu,
Sisi tumo mapenzini, tuache ya walimwengu,
Siogopi kukupenda, hata watu wakisema.


Mpenzi nakusifia, uzuri wa malaika,
Urembo ulozidia, hakika umeumbika,
Nami ninajivunia, kwako wewe nimefika,
U pekee duniani.

Hakika we u mzuri, kwa sifa zenye kujaa,
Kama nyota alfajiri, maishani unang'aa,
Uzuriwo u dhahiri, hakuna anokataa,
U pekee duniani.

Unayo sauti tamu, nyoka kutoka pangoni,
Mejaa mashamshamu, utamu masikioni,
Huniletea wazimu, kusisimuwa moyoni,
U pekee duniani.

Una rangi asilia, yang'ara kama dhahabu,
Rangi iliyotulia, wengine yawapa gubu,
Sichoki kukusifia, wewe ndo wangu muhibu,
U pekee duniani.

Macho kama ya gololi, na mapole kama njiwa,
Sifa wazistahili, kwani umebarikiwa,
Leo nasema ukweli, wanifanya kunogewa,
U pekee duniani.

Mwendo wako wa kuringa, mrembo mwendo mwendole,
Moyo wangu waukonga, waujaza raha tele,
Nipo radhi kukuhonga, sikupate watu wale,
U pekee duniani.

Sifa zako zimezidi, wewe u nambari wani,
Wewe kwangu maridadi, mwingine simtamani,
Nakupa yangu ahadi, daima 'takuthamini,
U pekee duniani.

Wewe wanipa sababu, kufurahia mapenzi,
Wako ustaarabu, hakika nitakuenzi,
Kukutunza ni wajibu, udumu wetu upenzi,
U pekee duniani.

leo nataka kuzungumzia maneno ya mahaba, jamani tunajuwa ya kwamba ukiwa na mpenzi wako unafurahi zaidi pale japo muda fulani atakupa maneno matamu, na mazuri na yenye kuzidi kukupa moyo wa wewe kuzidi kutaka kuwa naye...

sasa kuna wapenzi wengine hata mimi nilishapitia mmoja wakati fulani, jamani wanaume na wanawake wenzangu hebu tujitahidi maneno kama mpenzi, honey, sweety, mkiwa mbele za watu kumuita mpenzi wako sio mbaya maana wengine haswa waliozaa utasikia baba fulani mara mama fulani inamaana baada ya kuzaa mpenzi, sweety, honey umeisha?????? tunawapenda sana watoto wetu lakini wao wananafasi yao na mwenza wako ananafasi yake...

kwenye sita kwa sita watu utawakuta kimya tu madai wanasikilizia uhondo, jamani kuna maneno pale ama mnaoneana aibu sasa kwangu raha mpenzi aongee aniambie anavyojisikia wapi niongeze, vipi nikae, wapi nimshike kwa sauti ya taratibu na yenye mapenzi tele....sijui wewe mwenzangu

sasa pakiwa kimya tu jamani na ndio kwa mfano kitanda ndio vileeee ukigeuka tu majirani mpaka watujuwa hizo kwinyo kwinyo kwinyo hapo kwenye mechi sindio balaa maana utakuwa usikilizii raha unakilaani kitanda tu hichi nacho mpaka watu wajuwe leo napewa.....

kama mnaona aibu kuongea basi kama chumbani kuna redio wekeni hata mziki wa taratibu kuwahamasisha zaidi, maana ule ndio utakaoongea kwa niaba...

maneno ya mahaba jamani ndio mafuta tosha ya kuendesha hilo gari la mapenzi...


3 comments: